June 2026

Yohana 17:22-23 - 24-06-2026

Jumatano asubuhi tarehe 24.06.2026;

Yohana 17:22-23
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.

23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.

Waefeso 4:15-16 - 23-06-2026

Jumanne asubuhi tarehe 23.06.2026

Waefeso 4:15-16
15 Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo.

16 Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo.

Yeremia 35:12-19 - 20-06-2026

Jumamosi asubuhi tarehe 20.06.2026;

Yeremia 35:12-19
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema,

13 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Enenda ukawaambie wana wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, Je! Hamtaki kupokea mafundisho, myasikilize maneno yangu? Asema Bwana.

14 Maneno ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, aliyowaamuru wanawe, kwamba wasinywe divai, yametimizwa, na hata leo hawanywi; maana waitii hiyo amri ya baba yao; lakini mimi nimesema nanyi, nikiamka mapema na kunena, bali ninyi hamkunisikiliza mimi.

Waefeso 3:10-13 - 22-06-2026

Jumatatu asubuhi tarehe 22.06.2026

Waefeso 3:10-13

10 ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme na mamlaka katika ulimwengu wa roho;

11 kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu.

12 Katika yeye tunao ujasiri na uwezo wa kukaribia katika tumaini kwa njia ya kumwamini.

13 Basi naomba msikate tamaa kwa sababu ya dhiki zangu kwa ajili yenu, zilizo utukufu kwenu.

Pamoja tujenge Kanisa la Bwana;

Matangazo ya usharika tarehe 14 Juni 2026

DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI  

MATANGAZO YA USHARIKA TAREHE 14 JUNI, 2026 

SIKU YA BWANA YA 2 BAADA YA UTATU

NENO LINALOTUONGOZA NI:

“YESU NI MLANGO WA KUINGIA MBINGUNI”

1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli. 

2. Wageni: Hakuna Mgeni aliyetufikia na cheti: 

3. Matoleo ya Tarehe 07/06/2026

Tunamshukuru Mungu aliyetupa afya ya kumwabudu na utayari wa kumtolea kwa hiari mali alizotupa kwa kazi yake.

NAMBA YA SADAKA KWA NJIA YA MTANDAO: